-
Habari za Saa, Saa Nane na Dakika 55, Machi 04, 2021. - 54 mins ago
-
Umuhimu wa wanawake katika uchumi wa viwanda - about 1 hour ago
-
Saluni zafunguliwa tena Ujerumani - 2 hours ago
-
Habari za Saa, Saa Saba na Dakika 55, Machi 04, 2021. - 2 hours ago
-
COASTAL UNION Vs YOUNG AFRICANS UWANJA WA MKWA KWANI TANGA: UBOVU WA YANGA NI UMALIZIAJI - 3 hours ago
-
Taarifa ya Habari ya Radio One Saa Saba Mchana, Machi 04, 2021. - 3 hours ago
-
Habari za Saa, Saa Sita na Dakika 55, Machi 04, 2021. - 3 hours ago
-
SIMBA SC Vs AL- MERREIKH SPORTING CLUB: NI MECHI YA VITA, DO OR DIE, UCHAMBUZI - 4 hours ago
-
Habari za Saa, Saa Tano na Dakika 55, Machi 04, 2021. - 4 hours ago
-
MEDDY CLASSIC, MSANII CHIPUKIZI ALIYEMUIMBISHA RAPPER MAARIFA SINGELI/WASANII KUWASHIKA MKONO - 4 hours ago
ISHU YA UHABA WA MAFUTA YAMUIBUA WAZIRI WA KILIMO “CHANZO NI CORONA”
Waziri wa Kilimo Prof.Adolf Mkenda amesema uhaba wa mafuta ya kula kwa sasa umesababishwa na changamoto ya ugonjwa wa Corona duniani.
Prof.Nkenda ameyasema hayo mara baada ya kufanya ziara kwenye baadhi ya viwanda vya kutengeneza mafuta ya kula vinavyotumia malighafi za kilimo kuyaandaa.
Katika hatua nyingine Prof.Nkenda amewataka wakulima kuhakikisha wanatumia hali hii ya uhaba wa mafuta kujikita katika kilimo cha mimea inayotoa bidhaa ya mafuta ya kula kwani kwa sasa Tanzania inazalisha asilimia 47 tu za mafuta wakati serikali inatumia nusu trilioni yakuagiza mafuta kutoka nje ya nchi.
Katika hatua nyingine amesema serikali haijakataza kuuza mafuta ghafi nje ya nchi na kwa wale wayakaowazuia wawekezaji kiwekeza kwenye viwanda vya mafuta watachukulia hatua kali kisheria.